Monday 10 March 2014

ANGALIA BARABARA YA SAKOTA, TEMEKE ILIVYOBOMOKA NA KUHATARISHA WAPITAJI WA VYOMBO VYA USAFIRI

Dereva wa lori akilikwepa shimo litokanalo na kukatika kwa barabara ya Sakota wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam. Wakazi wa eneo hilo wamesema kwamba barabara hiyo iliharibika tangia desemba mwaka jana huku wakala wa barabara nchini(Tanroads) wakitembelea eneo hilo bila kuchukulia hatua zozote za ukarabati.
Barabara hiyo ikiwa imeharibika kwa kiasi kikubwa hivyo kuhatarisha wapitaji wa vyombo vya usafiri.

Dereva pikipiki akimuangalia dereva lori kwa kuhofia kubanwa upande wa shimo ambapo barabara ya Sakota, Temeke imeharibika.

No comments:

Post a Comment