Tuesday 11 March 2014

WAZEE WA YOMBO KILAKALA WATOA YA MOYONI

Mhasibu wa Kampuni ya Uwakala wa ajira ya Erolink, Joyna Mwafute akimlisha  chakula mmoja wa wazee waishio katika kituo cha Tushikamane Pamoja Foundation kilichopo Yombo kilakala Bi.Tabu Juma( 65) wakati  wafanyakazi wa kampuni hiyo walipofika kituoni hapo kutoa misaada wa vyakula,mafuta ya kula,blanketi na mashuka vyote vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 2.5/-.
Baadhi ya wafanyakazi wa Kampuni ya Uwakala wa ajira ya Erolink  wakiwa katika picha ya pamoja na wazee wasiojiweza wa kituo cha Tushikamane Pamoja Foundation ilichopo Yombo Kilakala wakati walipokwenda kuwapa msaada wa vitu mbalimbali vikiwemo mashuka, blanketi,vyote vyenye thamani ya zaidi ya shilingi Milioni 2.5/-.

.......................................................................................
WAZEE WALIA NA SERIKALI
 
Wazee wa Yombo Kilakala wameililia Serikali juu ya kukosa huduma stahiki kama ukosefu wa matibabu na matunzo bora kwasababu ya kunyanyapaliwa na kutelekezwa  na familia zao hivyo kuishi katika mazingira magumu.

Kauli hiyo imetolewa mwishoni mwa wiki na wazee waishio Yombo Kilakala wilayani Ilala jijini Dar es salaam  wanaofadhiliwa na Taasisi ya Tushikamane pamoja walipotembelewa  na Wafanyakazi wa kampuni ya Uwakala wa Ajira ya Erolink  kwa lengo la kukabidhi misaada mbalimbali ya kibinadamu yenye zaidi ya shilingi milioni 2.5/-.
 
Akizungumza kwa niaba ya wazee wenzake, Bi.Julietha Mchanga(90) alisema kuwa  changamoto kubwa nyowakabili ni  kukosa matunzo na matibabu yasiyostahili kwani wengi wao hawana msaada.
 

Bi. Mchanga alibainisha kuwa hayo yanatokana na kukimbiwa na  kutothaminiwa na watoto wao hivyo kukosa matunzo jamboa mabalo huwafanya wazee waishi maisha magumu.
 
Vilevile alisema kuwa sera ya kutunza wazee haitekelezwi ipasavyo hivyo ni wakati mwafaka kwa serikali na jamii kwa ujumla kutambua na kuwakumbuika kwani ni miongoni mwa watu waliosahaulika hapa nchini.
 
Mfanyakazi wa  Kampuni ya Uwakala wa ajira ya Erolink, Zabida Kibiki akimvisha shuka baada ya kumkabidhi msaada huo John Shitundu ambaye ni miongoni mwa wazee waliopo chini ya kituo chaTushikamane Pamoja Foundation wakati  wafanyakazi wa kampuni hiyo walipokwenda kutoa misaada mbalimbali kwa wazee hao wanaoishi katika kituo hicho kilichopo Yombo Kilakala jijini Dar es Salaam. Jumla ya vitu mbalimbali vilitolewa  ikiwemo mashuka ,blanketi , mchele na mafuta ya kupikia chakula vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 2.5. Kushoto anayeshuhudia ni Mwenyekiti wa kituo hicho Rose Mwapachu.
Kwa upande wake, Taddious Ndyetabuula  ambaye ni Meneja mikataba wa kampuni ya Erolink Alisema kuwa  msaada walioutoa  kwa wazee hao  umekwenda sambamba na maadhimisho ya siku ya wanawake duniani lakini pia lengo kuu ni kujumuika na  wazee wasiojiweza  ili  wajione kwamba hawajasahaulika.
 
“Msaada huu wa vyakula,mafuta ya kupikia ,sabuni  na mashuka pamoja na hafla hii ya  kujumuika na wazee kwaajili ya chakula cha mchana ni endelevu ,hivyo sisi kama Erolink ni jukumu na wajibu wetu  kuhakikisha kwamba tunawasaidia na kuwathamini wazee wanaoishi katika mazingira magumu” alisisitiza Ndyetabuula.
 
Baadhi ya wazee wanaoishi na kutunzwa katika Kituo cha  Tushikamane Pamoja Foundation kilichopo Yombo Kilakala jijini Dar es Salaam,wakicheza pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa kampuni ya Uwakala wa ajira ya Erolink  walipowatembelea wazee hao mahususi kwa kutoa msaada wa vitu mbalimbali kama vile mashuka ,blanketi , mchele na mafuta ya kupikia chakula vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 2.5/-.

Naye  Mwenyekiti  wa taasisi ya  Tushikamane Pamoja, Rose Mwapachu alisema kuwa  hana budi kuishukuru Kampuni ya Erolink kwa msaada walioutoa kwa wazee haoo lakini pia alitumia fursa hiyo kuyaomba mashirika na makampuni mbalimbali kuwaungamkono katika jitihada zao za kuhakikisha    ustawi wa maisha bora ya  wazee hapa nchini.
 
“Tuna utaratibu wa kutoa misaada ya kibinadamu  kwa wazee katika vituo mbalimbali jijini hapa ikiwemo kinondoni,manzese,tandale,magomeni na maeeo mengine lakini uwezo wetu ni mdogoi tunahitaji wafadhili zaidi kwaajili ya  kujenga majengo kuishi hawa wazee kwani wengine hawana makazi iantubidi kuwalipia kodi”Alisisitiza Mwapachu
 
Aliongeza kuwa hivi  sasa serikali imewapa kiwanja huko Kwembe (Nje kidogo ya jiji la Dar es salaam)na wapo katika hatua za mwisho za kuanza ujenzi  lakini pi8a bado wanahitaji msaada zaidi iliwaweze  kukamilisha ujenzi huo ili waweze kuwatunza na kuwalea  wazee  katika mazingira mazuri.

No comments:

Post a Comment