Monday 24 February 2014

Tigo yazindua huduma ya kwanza duniani ya kutuma na kupokea pesa kwa njia ya simu kimataifa, baina ya Rwanda na Tanzania, yenye uwezo wa kubadilisha fedha za kigeni

Balozi wa Rwanda nchini Tanzania Dr. Ben Rugangazi akionyesha meseji katika simu mara baada ya kupokea pesa kutoka Tigo Cash Rwanda. Kulia akionyeshea alama ya dole ni Mkurugenzi Mkuu wa Tigo Tanzania Diego Gutierrez. Hivi sasa wateja wa Tigo Tanzania wanauwezo wakutuma na kupokea pesa kutoka Tigo Rwanda bila makato yoyote.
Mkurugenzi Mkuu wa Tigo Tanzania Diego Gutierrez (kushoto) akifurahi mara baada ya kutaarifiwa kwamba muamala wa Tigo Pesa umepokelewa nchini Rwanda. Kwenye luninga (upande wa kushoto) ni Balozi wa Tanzania nchini Rwanda Francis Mwaipaja aliyepokea pesa hizo. Huduma hii inamwezesha mteja kupokea pesa moja kwa moja katika sarafu ya nchi yake husika na kuondokana na usumbufu wa kwenda kubadilisha fedha za kigeni.
..........................................................................................................................................
Dar es Salaam, Tanzania; Kigali, Rwanda: 24 Februari, 2014 – Tigo, kampuni ya mawasiliano ya kimataifa inayomilikiwa na Millicom (Stockholmsbörsen: MIC) ambayo ni kampuni inayoongoza katika nchi 13 barani Afrika na Amerika Kusini, imekuwa kampuni ya kwanza duniani kuanzisha huduma ya kutuma na kupokea pesa baina ya nchi mbili tofauti ambazo ni Tanzania na Rwanda.
 
Huduma hii mpya ilizinduliwa katika tafrija mbili tofauti kwa wakati mmoja ambazo zilifanyika katika miji ya Dar es Salaam na Kigali ambapo Balozi wa Rwanda nchini Tanzania Dr. Ben Rugangaza na Balozi wa Tanzania nchini Rwanda Bw. Francis Mwaipaja ndio walikuwa wa kwanza kufanya miamala ya kutuma na kupokea pesa kupitia njia ya simu kati ya nchi hizo mbili.
 
Huduma hii inatoa fursa kwa watumiaji wa Tigo nchini Tanzania kutuma pesa kwa njia ya simu kwa kutumia huda ya Tigo Pesa kwenda kwa watumiaji wa Tigo nchini Rwanda, na kinyume chake. Huduma hiyo inaweza ikabadilisha fedha za kigeni moja kwa moja, ambapo pesa inayotumwa kwa shilingi za kitanzania au francs za Rwanda zinaweza zikabidilishwa kuwa fedha za nchi zinakopokelewa.  
  
Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mkuu wa Tigo Tanzania, Diego Gutierrez, aina hii ya huduma ni ya kwanza duniani kwa kuwa na uwezo wa kubadilisha fedha za kigeni kutoka kwa mtumaji hadi kwa mpokeaji.
 
Fedha ikishapokelewa kwenye simu, mteja anaweza kuitumia kulipia huduma zote zinazopatikana kwenye Tigo Pesa au Tigo Cash iliyopo Rwanda. Hii inajumuisha kuongeza salio, kulipia bili ya maji, TV pamoja na usafiri, kuhamisha fedha kwenda kwenye akaunti za benki, kutoa fedha kutoka kwa wakala yeyote nchini pamoja na kutuma kwa urahisi fedha kwa watumiaji wengine wa Tigo Pesa.
 
Kutuma fedha kutoka Tigo Pesa (Tanzania) kwenda kwa watumiaji wa Tigo Cash (Rwanda), mteja anachotakiwa kufanya nia kupiga nambari *150*90#, huku wale walioko Rwanda wakipiga nambari *200*7#. Huduma hii inaweza ikatumika kutoka kwenye simu aina yeyote iliyounganishwa na laini ya Tigo. Wateja wa nchi husika watapokea fedha zao pale pale wanapotumiwa na kupokea katika aina ya fedha ya nchi husika.
 
Kujisajili kwenye huduma ya Tigo Pesa au Tigo Cash, wanachotakiwa kufanya wateja ni kutembelea wakala yeyote nchini Tanzania au Rwanda. Kujisajili ni bure. Kinachohitajika ni kitambulisho cha mhusika.
 
Kwa mujibu wa Gutierrez, “Huduma hii mpya itaokoa muda mwingi wa wateja pamoja na fedha zao. Watumaji wa fedha kimataifa wamekuwa wakienda sehemu za kubadilishia fedha za kigeni kuweza kubadilisha Francs za Rwanda kuwa dola kasha kutuma hizo dola kupitia kwa mawakala wengine wa fedha. Hivi sasa wanaweza wakatuma pesa kupitia simu zao.”
 
Gutierrez aliendelea: “Tunafurahi kuwapa wateja wetu nyenzo za kufanya miamala kwa wana Afrika mashariki wenzao. Tunashukuru kwamba kutokana na teknolojia yetu ya kisasa, wananchi wa Rwanda wanaweza kutuma pesa kwa familia, marafiki, pamoja na wafanyabiashara wenzao walioko nchini kwao.”
 
Tongai Maramba, Mkurugenzi Mkuu wa Tigo Rwanda naye alisema: “Tumefurahi kuanza kuwapa wateja wetu wa Tigo Cash uwezo wa kutuma fedha kimataifa kupitia simu zao. Pia ni jambo zuri zaidi kwamba wateja wetu wamerahisishiwa kwa kuweza kupokea moja kwa moja katika Francs za Rwanda kwa sababu kampuni nyingi za kutuma na kupokea fedha huwa wanatumia dola. Huduma hii haimpi wasi wasi wowote mteja kuanza kutafuta sehemu ya kubadilishia fedha.”
 
Murenzi Abdallah, msafirishaji anayefanya kazi katika kampuni moja ya usafirishaji kutoka Dar es Salaam kwenda Kigali na Goma alisema: “Nimefurahishwa sana na uwezo tuliopewa wa kutuma na kupokea pesa kwa njia ya simu nikiwa nchini Tanzania. Maisha yangu yatarahisishwa kwa namna ya kukamilisha kulipia ushuru mbali mbali mpakani pamoja na mahitaji mengine nikiwa katika safari zangu ndefu.”
 
Millicom inatoa huduma za kutuma na kupokea fedha nchini Tanzania, Ghana, Rwanda, DRC, Chad, Bolivia, Colombia, El Salvador, Guatemala, Honduras, Senegal na Paraguay, pia ina mpango wa kuzidi kupanua wigo wake katika nchi zingine katika siku za usoni.  
 
Huduma hii mpya ina manufaa makubwa kwa biashara zinazofanyika kati ya nchi hizi mbili, familia zinazokaa katika nchi hizi kama wageni, waendesha malori, wanaosafirisha na kununua bidhaa kutoka nchi zote mbili. Tanzania ni nchi ya pili inayoongoza kwa kufanya biashara na Rwanda. Mwaka 2013, Rwanda ilinunua bidhaa zenye thamani ya dola 80,883,702 kutoka Tanzania, huku bidhaa zinazoingizwa Tanzania zikithaminiwa kuwa dola 231,695,265 kutoka Rwanda mwaka huo huo. 

Balozi wa Rwanda nchi Tanzania Dk. Ben Rugangazi akitoa hotuba yake mbele ya waandishi wa habari na wageni waalikwa. Balozi Rugangazi aliipongeza kampuni ya simu ya Tigo na alisema kwamba huduma hiyo mpya ya kutuma na kupokea pesa itaweza kukuza uchumi wa nchi za Tanzania na Rwanda pamoja na kuendeleza kuimarisha ushirikiano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).
Waandishi wa habari na wageni waalikwa mbali mbali wakiwemo wafanyabiashara na wanafunzi wa Rwanda wanaofanya shughuli zao nchini.

No comments:

Post a Comment